MAABARA ZA KANDA ZABORESHWA. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, August 31, 2017

MAABARA ZA KANDA ZABORESHWA.


Kaimu Meneja Masoko, Mawasiliano na Huduma Kwa Wateja Cletus Mnzava akiwa upande kushoto akizungumza jambo katika Mkutano na waandishi wa habari, mwengine ni Afisa habari Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Sylvester Omary.
WINGU LA HABARI
Mamlaka ya Maabara ya Mkemia wa Serikali imeanza kuimarisha Maabara zote za kanda kwa lengo la kuwasogezea karibu huduma wananchi ambao awali walikuwa wanalazimika kufata kwenye Ofisi za Mkemia Mkuu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa habari Kaimu Meneja Masoko, Mawasiliano na Huduma kwa Wateja Cletus Mnzava, amesema kuwa hapa nchini kuna Maabara sita za kanda.
Manzava amesema kuwa kanda hizo ni pamoja na kanda ya ziwa inayohudumia mikoa ya Mwanza, Bukoba, Simiyu, Mara, Shinyanga, Geita na Kigoma.

Kanda ya Kaskazini inayohudumia Mkoa wa Arusha, Kilimanjaro, Tanga pamoja na Manyara, Kanda ya kati inayotoa huduma Mkoa wa Dodoma, Singida, Morogoro, Tabora na Iringa.

Kanda ya Mashariki inayohudumia Mkoa wa Dar es Salaam pamoja Pwani wakati kanda ya Nyanda za juu kusini inajumuisha mikoa wa Mbeya, Katavi, Songwe na Rukwa.
Kwa upande wa kanda ya Kusini itaendelea kuhudumia mkoa wa Lindi, Mtwara pamoja na Songea.

Amesema kuwa kwa sasa mamlaka imejipanga kuimarisha utendaji kazi wa kanda zake kwa kuzipatia vifaa vya maabara vya kisasa kwa kanda ambazo tayari zina maabara.

“Tutajenga majengo ya kudumu ya Ofisi za Mamlaka ya maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali katika kanda ili kuweza kuwekeza vifaa vya kudumu katika ofisi hizo badala ya sasa hivi inakuwa ngumu kwani muda mwingine unaweza kuweka mitambo ambayo mtatakiwa kuhamisha” amesma Mnzava.

Amesema kuwa lengo kuu la kuimarisha Maabara za kanda ni kusogeza huduma kwa wananchi na kuweza kuhudumiwa bila kulazimika kuja kufata baadhi ya huduma kwenye Ofisi za Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here