Watanzania wanatakiwa kuwekeza katika soko la hisa DSE. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, May 30, 2016

Watanzania wanatakiwa kuwekeza katika soko la hisa DSE.

Na mwandishi Wetu
Idadi ya mauzo katika soko la hisa imeongezeka kwa asilimia 76% kutoka Sh billion 2.8 hadi kufikia bilioni 4.9.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa mauso wa soko la hisa (DSE) Patrick Mususa, alisema kuwa idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa kwa wiki hii imeshuka kwa asilimia 20% hadi kufikia Sh Milioni 2.2 kutoka Sh Milioni 2.8 kwa wiki iliyopita.

Hata hivyo alibainisha kuwa  Kampuni tatu yanayohongoza kwa idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa ni pamoja na benki NMB kwa asilimia 48% , CRDB kwa asilimia 38% pamoja na kampuni ya SWISSPORT kwa asilimia 10%.

Aidha ukubwa wa mtaji wa soko umeongezeka asilimia 0.5% hadi kufikia sh Trilioni 22.1 kutoka sh Trilioni 22, Katika mtaji wa makampuni ya ndani umepungua kwa asilimia 0.1% hadi kutoka shTrilioni 8.4 hadikufikia  Trilioni 8.5.

Katika Viashiria Sekta ya huduma za kibenki na kifedha wiki hii imeshuka kwa pointi 10.36 baada ya bei kushuka kwenye kaunta za CRDB benki 1.33% na Sekta ya huduma za kibiashara (CS) wiki hii imeshuka kwa pointi 16.75 baada ya bei kushuka kwenye kaunta ya SWISSPORT (0.59%).

Akizungumzia Shindano la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu (DSE Scholar Investment Challenge 2016) Bw Msusa alisema kuwa Maendeleo ya Shindano hilo  yanakwenda vizuri na hadi sasa kuna idadi wanafunzi 3,160 kutoka vyuo mbali mbali ambao wanaendelea na ununuzi na uuzaji wa hisa na bondi katika DSE Scholar Investment Challenge 2016.

Katika shindano hilo kuna Vyuo vitano (5)  ambazo  vinavyoongoza kwa idadi ya wanafunzi waliofikia mia tano bora (Top 500) kwenye shindano hilo. Vyuo hivyo  ni pamoja IRDP DODOMA - inaongoza na wanafunzi 75, SAUT - inafwata na wanafunzi 66,UDSM - inafwata na wanafunzi 50 pamoja na IFM ikiwa na  wanafunzi 43.

Katika hatua nyingine DSE inaendelea kuuza hisa zake ambapo mtu yoyote  anaweza kununua na kuuza kwani hisa moja inauzwa kuanzia sh 500 na mtu anaruhusiwa  kununua hisa hadi 100.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here