Na Mwandishi Wetu
Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam, Meneja Masoko wa Dar Brew, Oscar Shelukindo alisema, bia hiyo iliyopo katika chupa nzuri ya plastiki inayovutia, itauzwa kwa bei ya Sh 1,000 tu kwa kila chupa.
“Leo ni siku ya furaha
kubwa sana kwetu Dar Brew na kwa watumiaji wote wa bia, kwani tumefanikiwa
kuzindua chupa hii itakayouzwa kwa bei nzuri ya Sh 1,000 tu na kwa ujazo
unaotosheleza” alisema.
Shelukindo alibainisha kuwa Bia hiyo imetengenezwa kwa utaalam wa
hali ya juu na kwa kutumia mitambo ya kisasa kabisa, na kuhakikishia watumiaji wanatumia
bei ikiwa na ubora wa hali ya juu.
Shelukindo alisema, bia hiyo imetengenezwa kwa kutumia malighafi
za hapa nyumbani, ikiwemo nafaka ya mtama ulio bora, hivyo kuna kila sababu
kwa Watanzania kujivunia kilicho chao na kukumbuka asili yao, kwani hii ni bia
yao ya asili.
“Chibuku Super ina kilevi cha asilimia 4, kinachokufanya uitumie
kwa muda mrefu ukiwa na marafiki, lakini inakupa lishe nzuri kutokana na
virutubisho vinavyopatikana katika nafaka zilizotumika kutengeneza bia hii.”
Naye Meneja Mauzo na Usambazaji wa Dar Brew, Fred Kazindogo
alisema, bia hiyo itaanza kupatikana nchi nzima katika baa, maduka makubwa
(Super Markets), katika maduka ya jumla na rejareja na sehemu zinazouzwa vileo
kuanzia leo.
“Tunatarajia wateja na wapenzi wa bia wataifurahia chupa hii mpya
na kwa wauzaji wa jumla, tunaamini watahamasika kuuza Chibuku Super kwani ina
faida nzuri na haina usumbufu wa kununua chupa,” alisema.
Kazindogo alisema, ana imani kubwa wapenzi wa bia wataipokea kwa
shangwe na wataitumia ili kuonesha wanajali asili yao.

No comments:
Post a Comment