Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
TIMU ya Taifa ya mpira wa mikuu Tanzania ''taifa stars'' wanatarajia kushuka dimani juni 4, mwaka huu kuminyana na Mapharao wa Mirsri katika mchezo wa kutafuta nafasi ya kushirika michuano ya kombe la mataifa Afrika (AFCON) ambao utapigwa majira ya saa 10 jioni katika uwanja wa taifa uliopo jijini Dar es Salaaam.
![]() |
| Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania 'taifa stars'' ambacho kinatarajia kushuka dimbani hivi karibuni kuminyani na Mapharao wa Misri jijini Dar es Salaam. |
TIMU ya Taifa ya mpira wa mikuu Tanzania ''taifa stars'' wanatarajia kushuka dimani juni 4, mwaka huu kuminyana na Mapharao wa Mirsri katika mchezo wa kutafuta nafasi ya kushirika michuano ya kombe la mataifa Afrika (AFCON) ambao utapigwa majira ya saa 10 jioni katika uwanja wa taifa uliopo jijini Dar es Salaaam.
Katika mchezo huo utakaochezeshwa na marefa wanne
kutoka Gabon ambapo mwamuzi wa kati
atakuwa ni Meye Bastrel atakayesaidiwa na Mihundou Ganther na Vinga Theophile
wakati Mwamuzi wa akiba (mezani) atakuwa Otogo Eric.
Laikini Kamishna wa mchezo huo ni Tarig Atta Salih kutoka Sudan.Maandalizi ya mchezo huo
yamekamilika kwa Shirikisho Soka la Tanzania (TFF) kuipokea timu ya taifa ya
Misri inayotarajiwa kuingia leo ambapo wataweka kambi kambi kwenye Hoteli ya
Kilimanjaro Kempiski, Dar es Salaam.
Taifa Stars imeweka kambi Hoteli Urban Rose ambayo pia iko katikati ya jiji la Dar es Salaam tangu iliporejea kutoka Kenya jMei 30, 2016 ambako ilicheza timu ya Taifa ya Kenya maarufu kama Harambee Stars. Katika mchezo huo uliofanyika Jumapili Mei 29, mwaka huu timu hizo zilitoka sare ya 1-1.
Wakati huo huo: Timu ya soka Taifa ya Wanawake ya Tanzania – Twiga Stars, inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Rwanda, utakaofanyika Uwanja wa Amahoro jijini Kigali, Rwanda.
Rwanda wameomba mchezo ufanyike ili kukiimarisha kikosi chao pamoja na kuboresha uhusiano wa nchi ambazo zote ni nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

No comments:
Post a Comment