Aliyepanga shambulio la chuo kikuu cha Garissa auwawa - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, June 2, 2016

Aliyepanga shambulio la chuo kikuu cha Garissa auwawa

Kamanda  wa  ngazi  ya  juu  wa  kundi  la  al-Shabaab anayeshitakiwa  kupanga  mashambulizi  ya  mwaka  2015 dhidi ya  chuo  kikuu  cha  Garissa  nchini  Kenya  ameuwawa  katika shambulio  la  majeshi  maalum kusini  mwa  Somalia.
Serikali  ya  Kenya  imesema  Mohammed Kuno  alihusika  katika kupanga  shambulio  la  Aprili  2015  ambalo  lilisababisha  vifo vya  watu 148.
Operesheni  hiyo , iliyofanywa  na  wanamgambo  wanne  wa  al-Shabaab , ilikuwa  shambulio  baya  kabisa  la  kigaidi  nchini Kenya tangu  pale  al-Qaeda  waliposhambulia  ubalozi  wa Marekani mjini  Nairobi mwaka  1998, na  kuuwa  watu 213.
Chanzo DW.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here