Ujenzi wa ghorofa wamponza aliyekuwa Mwenyekiti CCM. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, May 18, 2016

Ujenzi wa ghorofa wamponza aliyekuwa Mwenyekiti CCM.

Na Mwandishi wetu
KESI  inayomkabili aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Kilimanjaro ,Thomas  Ngawaiya juu ya kujenga ujenzi wa ghorofa bila kufata sheria, Kesi hiyo imeendelea leo katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu iliyopo jijini Dar es Salaaam.

Wakili upande wa utetezi, Jonathan Mulinga ameitaka mahakama isizogeze mbele kesi hiyo ile wamalizane na upande wa mashtaka kwa kujadiliana na kupata muafaka nje ya mahakama hiyo.

Hata hivyo Hakimu Mkazi  Respicios Mwijage amehailisha kesi hiyo mpaka itakapotajwa tena  Juni 16 Mwaka huu.

Ngwaiya alifikishwa katika mahakama hiyo ya Hakimu  Mkazi Kisutu kwa kosa la kufanya shughuli za ujenzi wa ghorofa kinyume cha sheria namba 17 kifungu 22(4) ya ukandarasi ya mwaka 1997.

KATIKA hatua nyingine Mtu mmoja aliyefahamika kwa majina Mbaraka  Mtambo (50) amefikisha katika mahakama ya hakimu mkazi kwa kosa la kusafirisha nyara za serikali alizokamatwa nazo katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julias nyerere.

Akisoma mashitaka hayo na Wakili wa serikali Hanorin Mushi Wakili  mbele ya Hakimu Mkazi Helen Liwa amesema kuwa mtuhumiwa huyo Tarehe 7 Mei mwaka huu alikamatwa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julias Nyerere  na magamba mawili ya Kasa ambayo ni Mali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mshitakiwa amekiri kutenda kosa hilo, hivyo Hakimu Liwa alimwambia kuwa hatipata dhamana kutoka na kesi hiyo,  ambayo itatolewa uamuzi kesho tarehe 19 Mei.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here