LHRC Wasikitishwa na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, May 13, 2016

LHRC Wasikitishwa na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

Na Mwandishi wetu







Kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC), kimesikitishwa na vitendo vinavyofanywa na baadhi ya watu juu ya kusambaza picha za kutisha ikiwemo picha za marehemu katika vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii bila kijali kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

Haya yamebainisha  leo na Mkurungenzi Mtendaji (LHRC), Dkt Helen kijo Bisimba, ambapo amesema kuwa kumekuwa na matukio kadha yanayofanywa na watu juu ya kurekodi picha ambazo sio nzuri kwa mujibu wa sheria.

Dkt kijo amesema kuwa Mei 4 mwaka huu, katika Mkoa wa Pwani Wilaya ya Bagamoyo pisha za  Miili ya marehemu mama na mtoto ambayo majina yao yamehifaziwa,  zilisambazwa katika mitandao ya kijamii zikionyesha majeraha ya kutisha   kutokana  na kitendo cha kinyama walichofanyiwa.

Katika tukio la pili amebainisha kuwa ilitokea Mkoa wa Kilimanjaro mwaka huu, ambapo picha za maiti ya mtoto  aliyeuwawa na mama wa kambo zikionesha akiwa ndani ya jeneza.

Hata hivyo maeneo ya kibamba jiji Dar es Salaam, January mwaka huu Picha za utupu za mwanamke aliyesemekana kuwa ni msukule aliyekutwa kwenya kisima,na picha hiyo ilizambaza katika mitandao ya kijamii.

Amesema kuwa hayo ni baadhi ya matukio, hivyo jamii inapaswa kutambua  vitendo hivyo ni udhalilishaji na kinyume cha sheria, kwani kwa mujibu wa haki ya kikatiba ibara ya 16 ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya 1977  kila mtu ana haki ya kikatiba ya kuthamini utu  wake kwa kuwa faragha  akiwa hai au amefariki.




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here