Kocha wa klabu ya soka ya Chelsea Jose Mourinho amesema
bado hajaketi kuzungumza na wakurugenzi wa bodi ya klabu hiyo juu ya usajili
mwingine mwingine wa January mwakani ndani ya klabu hiyo.
Mourinho amesema anachokifanya kwa sasa ni kuhakikisha
anakiboresha kikosi chake katika kipindi hiki ambacho kwao ni kigumu.
Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu soka nchini Uingereza
wanahusishwa na usajili wa majira ya baridi mwakani kwa wachezaji wa Atletico
Madrid’s Antoine Griezmann, Harry Kane na Jamie Vardy.
“Tupo mwezi Novemba
hivi sasa na tunachokitazama kwa sasa ni kufanya kazi nzuri kadri
tunavyoweza na hatujaongea bado na bodi juu ya kuongeza wachezaji wengine ndani
ya klabu hii",Alisema Mourinho
No comments:
Post a Comment