WILLKOMEN JÜRGEN KLOPP KARIBU JÜRGEN KLOPP "THE NORMAL ONE" - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, October 15, 2015

WILLKOMEN JÜRGEN KLOPP KARIBU JÜRGEN KLOPP "THE NORMAL ONE"



Na Kelvin Lyamuya.

 Utaona fulana zenye picha ya mtu huyu zikichukua nafasi kubwa, Ndio. Utacheka kwa furaha pale utakapoona picha mitandaoni pamoja na video mbalimbali zilizotengenezwa kwa mfano wake. 

Na najua katika akili yako ni nini unachofikiria kwa sasa, maisha ya Liverpool chini ya Jürgen Klopp. Ndio kwanza akitimiza siku kadhaa tangu atangazwe rasmi kama mrithi wa Rodgers, Jürgen Klopp ameleta taswira mpya katika mioyo iliyojeruhiwa ya wana 'Kop' duniani kote, ilikuwa ni zaidi ya Shayiri nzuri kwenye kilevi cha ndugu zangu wa kule Marangu. 

Kama wachezaji wa Liverpool wataelewa nini akitakacho Klopp na kwa muda gani, basi amin nakwambia ile 'Golden sky' ambayo mashabiki 45,000 wanaiimba kila wikiendi pale Anfield wataifikia tena,haiko mbali sana ni kiasi cha kusubiri. Ingawa ameshaweka wazi kuwa mapambano ndio yanaanza sasa, Klopp, amewasili katika kipindi kigumu, Liverpool tayari imeshacheza michezo nane ya Ligi Kuu England, na asilimia 80 ya wachezaji wa kikosi cha kwanza wapo kwenye majukumu ya Taifa mpaka katikati ya wiki hii, na kama hiyo haitoshi Nahodha wa timu, Jordan Henderson naye ni majeruhi.

 Hakuna mechi za kirafiki ambazo zingemsaidia kupata aina na mfumo mzuri katika timu, dirisha la usajili nalo limefungwa labda angepata wachezaji wa kuweka sawa kikosi. Miezi miwili na nusu iliyobaki ni kuipa timu morali, kuwaelewa na kuwaweka pamoja, na wakati huo huo azoee mji mpya, tamaduni pamoja na Ligi kwa ujumla. Ni kazi ngumu kwa yeyote yule, hata kwa mtu wa kariba na kujiamini kama Klopp. Labda alikuwa sahihi kusema Liverpool ipo katika njia sahihi kwa kiasi fulani, lakini kuna sehemu mbalimbali zenye kasoro katika klabu zinatakiwa kurekebishwa na muda ndio hivyo tena hautoshi kufanya yote hayo, huku kwetu wanategemea makubwa na inabidi wawe hivyo hivyo, Imani. Klopp amewasili katika kipindi ambacho mashabiki wa Liverpool wana manung'uniko kuona heshima ya klabu yao imeshuka, imekuwa kama kiroba cha kilo 20, Liverpool imekuwa nyepesi sana hivi karibuni na huo ndio ukweli wenyewe. Sina shaka naye, ameonyesha wazi jinsi gani heshima inavyotafutwa kwa njia yoyote ile, enzi za Signal Iduna Park.

 Ni muda wa kupambana kwa uhodari, kujitoa, na kufanya kazi kwa umoja, nikimaanisha 'Utatu Mtakatifu' wa mashabiki, wachezaji na kocha kuungana katika njia moja. Mafanikio. Katika kipindi cha miongo miwili iliyopita, mara kwa mara kulikuwa na kasoro katika sera ndani ya klabu pamoja na kutosikilizwa kwa mawazo ya wale wanaoamini kitu flani hakiendi sawa kwa hiyo kifanywe hiki, ilichangia katika kufifisha vitu viwili ambavyo ni MUHIMU katika klabu- matokeo ya uwanjani na furaha ya mashabiki.

 Soka imekuwa ni mchezo mgumu pengine kuliko kipindi cha nyuma, lakini bado yale mambo ya msingi yanatakiwa kufuatwa; klabu yoyote yenye mafanikio ni ile ambayo mawazo, malengo yameungana kwa pamoja hivyo kufanya kazi inakuwa ni rahisi, hakuna mizozano. 

Mashabiki wa Liverpool wamemuamini Klopp kwa asilimia zote, na wamempa muda wa kuwasilisha falsafa zake ndani ya Anfield. Tunaishi katika umri wa kutegemea makubwa bila kufikiri ni njia gani hasa ya kuyapata. Kwa ujio wa Klopp makubwa yanaweza kutokea. Pia atawafanya wachezaji wa Liverpool kuitumikia klabu kwa moyo wote, wakiwa chini ya kocha mwenye hadhi kama yeye hilo halina maswali. Kama kutakuwa na manung'uniko, uchovu kwa kipindi alichokuwepo Rodgers, basi katika kipindi cha wiki moja tu kila kitu kitakuwa sawa. Atawahitaji wachezaji kwa asilimia zote, ndio, watafanya kazi bila kuchoka kwa ajili ya kuleta kile wasemacho "Total Footbal", aina ya soka analolihusudu sana kocha huyu. Timu zinachocheza soka la kuvutia, zile zilizofanikiwa, hazitegemei bahati ila ni kuchapa kazi ndio silaha yao. 

Kama wachezaji wa Liverpool wanahitaji hisani, wanatakiwa kufanya kile Klopp anachokitaka, mchana na usiku. Kama wana wasiwasi kwamba ni kitu gani watakachokipata kama wakifanya kazi kwa umoja na bila kuchoka basi warudishe kumbukumbu nyuma, enzi Klopp anafundisha timu za Mainz 05 na Borussia Dortmund, kule anatajwa kama gwiji wa kuheshimika. Klopp wakati anahojiwa siku ya Ijumaa, kuna neno moja alisema ukilitathmini kwa umakini utaelewa, “Kuingia katika klabu sio jambo la muhimu sana kuwafanya watu wakufikirie, wafanye watu wakukumbuke pale unapoondoka." Wajerumani kadhaa walipita Anfield, wakafanikiwa, basi kama Klopp ni kama waliopita, Kops mpo katika njia moja ya mafanikio,Willkomen Jürgen Klopp.



                 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here