AJALI YAUWA WATU 42. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, October 23, 2015

AJALI YAUWA WATU 42.

Watu 42 wamefariki dunia baada ya basi waliopanda kugongana na gari la mizigo mashariki ya mji wa Bordeaux nchini Ufaransa.

Polisi nchini ufaransa wanasema magari yote hayo mawili yaligongana katika barabara moja ya mtaa wa Puissguin, kusini magharibi ya Ufaransa na kuripuka,  hivyo  wahanga 41 ambao walikuwa wazee waliokuwa wamejiandaa kwenda matembezi.

Hata hivyo  Dereva wa gari la mizigo lililokuwa limesheheni mbao,nae amefariki na Watu wanane wamefanikiwa kuyanusuru maisha yao-watano kati yao wamejeruhiwa katika ajali hiyo.


Kufatia ajali hiyo Mtumishi wa serikali ya mji huko Puisseguin amesema ajali hiyo imetokea leo katika eneo linalojulikana kuwa ni la hatari, na  kubainisha  kuwa ajali kama hiyo iliwai  kutokea miaka 30 iliyopita nchini humo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here