Waziri wa mambo ya nchi za nje
wa Marekani John Kerry na mwenzake wa Urusi Segej Lawrov wanakutana mjini
Vienna Austria kwa ajili ya kumaliza
vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria.
Nchi hizi mbili zina misimamo
tofauti kuhusiana na mzozo wa Syria ambapo Marekani inamtuhumu rais Bashar al
Assad kuhusika na matumizi ya nguvu dhidi ya wakazi wa nchi hiyo pamoja na
kuziendeya kinyume haki za binaadam.
Lakini Urusi ni mshirika mkubwa
wa Assad na wanataka kwa kila hali aendelee kuwepo madarakani uku Balozi wa
Marekani katika Umoja wa mataifa Samantha Power amekumbusha muda mfupi kabla ya
mazungumzo ya Vienna kuanza,kwamba wasyria 85 elfu wamefukuzwa pekee katika
kipindi cha siku chache zilizopita.
Baada ya mazungumzo
yao,mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani na Urusi watakutana kwa
mazungumzo ya pande nne pamoja na wenzao kutoka Uturuki na Saud Arabia.
No comments:
Post a Comment