WATANZANIA WANATAKIWA KUCHAGUA WAGOMBEA WENYE MASLAHI NA TAIFA. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, October 24, 2015

WATANZANIA WANATAKIWA KUCHAGUA WAGOMBEA WENYE MASLAHI NA TAIFA.

Watanzania wametakiwa kuchagua wagombea  katika nafasi ya Udiwani, Ubunge pamoja  na Urais wenye  vigezo vya kuongoza na  kujali maslahai ya taifa na sio chama chake.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Idara ya Kampeni na uchaguzi wa NCCR-MAGEUZI Faustin Sungura ambapo alisema kuwa wamefatilia  kwa umakini wa hali ya juu kampeni za uchaguzi wa wagombea wa vyama mbalimbali hapa nchini na kubaini baadhi ya wagombea hawakubaliani na sera za chama chake kutokana ufisaidi unaofanyika.

Sungura alisema kuwa kutoka na sera anazotumia  mgombea wa  Urais kupitia Chama  cha Mapinduzi CCM Dkt  John Pombe  Magufuli inonyesha kuwa hata yeye hapendi mwenendo wa chama chake.

Alisema mikutano yake ya kampeni ulezea maovu ya yanayofanya na Serikali CCM  kwani  baadhi ya mikutano hiyo alisema  kuwa  nikiwa Rais itakuwa mwisho serikali kuwakopa wakulima,kwa sababu ni aibu, nikiwa Raisi itakuwa marufuku wagonjwa kwenda hospitalini kuandikiwa dawa na  kuelekwezwa wakazinunue kwenye maduka  ya dawa.

Sungura alisema kuwa  katika hali  ya kawaida ,  maneno hayo au hutuba kama  hizo zilitakiwa kuchukuliwa  hatua na chama chake kutokana na ukimya wa chama,  Dkt Makufuli huenda angetekeleza yaliyo  moyoni mwake juu  ya chama chake.

‘’ Kutokana na sera za Dkt Magufuli za kuikosoa serikali ya CCM , hakuna sababu za msingi za kuendelea kuwachagua wagombea wa Chama cha Mapinduzi ,  badala yake tunawaomba wapiga kura wachague wagombea kutoka kambi ya upinzani’’ alisema.

Mbali na hayo Sugura amebainiisha kuwa kwa mujibu wa sheria mpiga  kura anahaki ya  kumchagua mgombea yoyote anayemtaka pamoja  na  kubaki au kuondoka kwenye eneo la  mduara wa mita 200 kutoka kwenye kituo cha kupiga kura.
Hata hivyo amefafanua kuwa kwa mujibu wa kifungu cha sheria ya uchaguzi 104(1), kinakataza kufanya kampeni, kuvaa sare ya chama,  au kufanya ishara inayoashiria kumfanyia  kampeni mgombea wa siasa, na  kifungu cha 126 cha sheria ya uchaguzi kinasema maelezo yoyote yanayokizana na sheria  yanayotolewa na tume ya uchaguzi ni  batili, na Maelekezo ambayo yasiyo halali  kwani yanalenga kuwaogopesha wapiga kura na kutoa mwanya kw Chama cha CCM kuchukua madaraka kwa kwa uwepesi.
 
Sanjali  na hayo alisema kuwa Mamlaka ya kituo cha kupiga kura yanaishia kwenye mipaka ya kituo cha  kupiga kura tu,na kifungu cha  sheria cha  104(1) cha uchaguzi  kinatoa eneo la mita 200 tu kutoka kituo cha kupiga kura, hivyo mtu yoyote akiamua kukaa nje  ya mita  200 bila kufanya fujo akiwa amekaa inakubalika  kwa mujibu wa sheria na hawezi kuhesabiwa kuwa amevunja sheria.

‘’ NCCR-Mageuzi hatupo tayali kuona baadhi ya watu wanatumia vibaya madaraka ya umma kukisaidia chama kuendelea kuwanyonya watanzania’’ alisema.

Sugura amewaomba watazania kwenda kupiga kura Oktoba 25 mwaka huu na kuchagua wagombea wa wote wa Umoja wa Katiba UKAWA katika ngazi ya Udiwani, Ubunge pamoja na Urais.










No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here