Waandishi wa
habari nchini wametakiwa kuandika habari za uchaguzi bila upendeleo
wowote,wakati huu wakampeni na wakati wa zoezi la uchaguzi utakaofanyika octoba 25 mwaka huu,ili kuliepusha taifa kuingia katika machafuko ya kisiasa.
Hayo
yamesemwa na mkurugenzi wa habari maelezo Assa Mwambene alipo kutana na
waandishi wahabari kuzungumzia mstakabali wa taifa katika kipindi hiki, ambapo ameleeza kuwa uchaguzi wa mwaka
huu umekuwa na mwamko ana ari kubwa kutoka kwa wananchi hivyo amewaassa kuzingatia maadili na miiko
ya kazi yao ili kila pande zipate haki sawa.
Aidha
Mmwambene amesema nchi nyingi jirani na Tanzania kama,Rwada ,Burundi na kenya
ziliingia katika machafuko huku riport
zikieleza kuwa machachafuko hayo kwa sehemu kubwa yalichangiwa na vyombo
vyahabari hivyo nivema kuitunza heshima
ya Tanzania kimataifa kwakuwa ina sifika kuwa ni kisima cha Amani na kimbilio
la nchi jiran.
Pamojana
hayo amewataka waandishi wa habari wa kimataifa kufuata taratibu za tume
yaTaifa ya uchaguzi zilizo wekwa ili kuondoa usumbufu utakao weza kujitokeza, na
pia amewatakawata watanzania kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kupata
viongozi wanaowataka na wadumishe Amani kwa muda wote wa zoezi hilo.
No comments:
Post a Comment