MBEYA CITY WAUNDA KAMATI MAALUM KUCHUNGUZA SAKATA LA JUMA NYOSSO. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, October 1, 2015

MBEYA CITY WAUNDA KAMATI MAALUM KUCHUNGUZA SAKATA LA JUMA NYOSSO.

Mchezaji wa Mbeya City Juma Nyosso









Uongozi wa Mbeya City, umeamua kuunda kamati maalum kwa ajili ya kuchunguza suala la beki na nahodha wake, Juma Said Nyosso.

Uamuzi huo umetokana na Nyosso kubainika akimtendea udhalilishaji nahodha wa Azam FC, John Bocco.

Taarifa zimeeleza, kamati hiyo itatoa majibu kesho kwa bodi ya jiji la Mbeya na baada ya hapo utaelezwa uamuzi wake.

Tayari shirikisho la mpira wa miguu  TFF imetoa adhabu kali ya miaka miwili kutocheza soka na faini ya Sh milioni mbili kwa Nyosso.

Lakini ajabu, pamoja na kuonekana kwenye picha akifanya jambo hilo, Nyosso ameanzisha kampeni za kukana jambo hilo.

Nyosso amekuwa akidai hakumbuki kufanya hivyo tena akinadai teknolojia inaweza ikawa inamhukumu.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here