WANANCHI MKOANI MOROGORO MAJONZI MAKUBWA,MAZISHI YA MH CELINA KOMBANI. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, September 29, 2015

WANANCHI MKOANI MOROGORO MAJONZI MAKUBWA,MAZISHI YA MH CELINA KOMBANI.



MWILI WA MAREHEMU  MH BI CELINA KOMBANI UKIWA UMEBEBWA
TAYALI KWA KUZIKWA

Wananchi wa mkoa wa Morogoro wamepokea kwa majonzi msiba wa aliyekuwa waziri wa nchi ofisi ya rais menejimenti ya utumishi wa umma na mbunge wa jimbo la Ulanga Bi, Celina Kombani mazishi yaliofanyika leo katika eneo la shamba lake lililopo Lukobe manispaa ya Morogoro.

Wakizungumza nyumbani kwa marehemu wakazi wa Morogoro wameeleza kusikitishwa na msiba huo ambapo wamesema marehemu alikuwa kipenzi cha watu, mchapa kazi na kuwataka wakazi wa Morogoro hususani wa jimbo la Ulanga kuwa wavumilivu kwa kupotelewa na kipenzi chao ambapo waziri huyo alikuwa anagombea ubunge kwa awamu ya tatu kwa tiketi ya CCM katika jimbo la Ulanga.

Wakizungumza kwa niaba ya familia kaka wa marehemu Martin Ombeshi na mkwe wa marehemu Bw, Jeradi Mlenge wamesema wameupokea msiba huo kwa masikitiko ambapo wameeleza mazishi hayo yamefanyika leo  mkoani Morogoro shambani kwake Lukobe


Waziri wa nchi ofisi ya rais menejimenti ya utumishi wa umma na mbunge wa jimbo la Ulanga Bi, Celina Kombani kipindi cha uwahi wake.
Waziri mkuu Mzengo Pinda akitoa salama za mwisho





No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here