| Meneja wa soko la hisa Patric Mususa. |
Idadi ya mauzo katika
soko la hissa (DC) imeongezeka mara tano kutoka bilioni mbili nukta moja hadi
kufikia bilioni 12.2 kwa wiki hii.
Akizungumza na wingu la habari jijini Dar es salaam Meneja wa soko
hilo Patric Mususa alisema kuwa katika soko hilo pia idadi ya hissa
zilizonunuliwa na kuuzwa imeongezeka mara sita kutoka milioni 1.4 hadi kufika milioni hadi kufukia milioni 9.1 kwa wiki hii .
Alisema kuwa Kampuni tatu zinazoongoza katika soko hisa
zake kununuliwa na kuuzwa ni pamoja na
Baki ya CRDB inayoongoza kwa 75.35%, TWINGA
CEMENT TPCC ikiwa na 21.81% uko TANAZANIA CIGARETTE TCC ikiwa na 1.38%
.
Sanjali na hayo idadi ya mtaji wa soko imeshuka kutoka kutoka
trilioni 221.1 hadi trilioni 21.8, wakati idadi ya mtaji wa makapuni ya ndani
imepanda kutoka trilioni 9.7 hadi kifikia trilioni 9.8.
Pia mabadiliko ya bei za hisa kampuni mbili zimeongoza katika ongezeko la bei ya
hisa zake ambazo ni TOL imeongezeka kwa asilimia 1.32, NATION MEDIA GROUP NMG
kwa asilimia 1.01.
Mbali na hayo Kiashiria cha sekta ya viwanda kimeshuka kwa nukta
55.44 kikiwa kimechangiwa na punguzo la bei ya hisa kwenye kaunta ya TBL kwa
asilimia 1.19 na TCCL (SIMBA CEMENT) kwa asilimia 2.63 .
Wakati kiashiria cha sekta ya huduma za kibenki na kifedha
kimeshuka kwa nukta 28.65 kikiwa kimechangiwa na punguzo la bei ya hisa kwenye
kaunta ya DCB kwa asilimia 2.5 na NMB
kwa asilimia 2.08 na kiashiria cha sekta ya huduma za kibiashara kimeshuka kwa
nukta 50 kikiwa kimechangiwa na punguzo la bei ya hisa SWISSPORT kwa hisa asilimia
1.60
Mususa amebainisha kuwa huduma ya kununua na kuuza hisa kwa
njia ya simu ya mkononi inaendelea vizuri kwa huduma kwa wananchi wote,
nakuwataka watu kuendelea kutumia huduma hiyo kwa kupiga *150*36#.
No comments:
Post a Comment