WANACHAMA WA CUF VISIWANI ZANZIBAR WAVUNJA KIOO CHA MBELE GARI LA CCM. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, October 5, 2015

WANACHAMA WA CUF VISIWANI ZANZIBAR WAVUNJA KIOO CHA MBELE GARI LA CCM.


Kaimu Katibu mkuu  wa VCCM .













Umoja wa vijana wa chama cha Mapinduzi (UVCCM) umewataka wanachama wa chama cha wananchi CUF visiwani zanziba kuacha vitendo vya uvunjifu wa Amani katika mikutano ya kampeni za siasa ya chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam Kaimu katibu mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka amesema kuwa kati ya septemba 15 hadi 18 mwaka huu misafara ya CCM katika maeneo ya Kuyuni, Mtuhaliwa  kwa chokocho katika mkoa wa kusini pemba umeshambuliwa kwa kupigwa mawe wakati wanachama wa CCM wakitoka kuhudhuria mikutano ya kampeni, na baadhi ya watu wamejeruhiwa na kupata majereha ikiwemo gari moja kuvunjwa kioo  cha mbele.

Pamoja na hayo Shaka amesema kuwa kuhama kwa mwanasaisa mkogwe Kingunge Ngombale Mwilu si jambo geni kwao kwani tayari walikwisha mvua ukada mkuu wa jumuhiya hiyo baada ya kutoridhishwa na mwenendo wake katika  chama.

Hata hivyo  amebainisha kuwa kuhama kwa Kingunge kunatokana na kutoheshimu matokeo ya michuano ya nguvu ya hoja ndani ya chama huku akitaka kulazimisha fikra zake zionekane sahihi za wenzake zikikosa maana na umuhimu wowote.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here