Shirikisho la Michezo la Mashirika ya umma na makampuni
binafsi Tanzania (SHIMMUTA) zimezitaka
timu zinazotarajia kushiriki bonanza la michezo Oktoba 10 mwaka huu , kushiriki kikamilifu ili
kuleta ushindani katika bonanza hilo.
Bonanza hilo ambalo limepagwa kufanyika katika viwanja vya
chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kuanzia saa 12 asubuhi hadi 12 jioni kwa
saa za afrika Mashariki.
Akizungumza na wingu la habari Katibu Mkuu wa SIMMUTA Award
Safari amesema kuwa maandalizi kwa
ujumla yamekwisha kamilika na zitaka timu
zote kufata ratiba ikiwemo kufika kwa wakati eneo la tukio .
Safari amebainisha kuwa
mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa taifa wa hifadhi ya jamii (NSSF )Ramadhani
Dau atakuwa mgeni rasmi katika bonanza hilo.
‘’Siku hiyo ya uzinduzi mgeni rasmi atakuwa Ramadhani Dau
ambapo hatazindua bonanza hilo lenye lengo ya kukuza michezo kwani michezo ni
afya na inajenga mwili ikiwemo kuepuka magonjwa ya mara kwa mara’’ alisema.
Katika bonanza hilo zinatarajiwa kushiriki Jumla ya timu 10 za
taasisi, mashirika ya umma pamoja na makampuni binafsi yaliyopo hapa jijini Dar
es Salaam ambapo yatahusisha wanamichezo wafanyakazi wa rika mbalimbali.
Timu ambazo zitashiriki katika bonanza hilo ni pamoja na
Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL). Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Chuo cha
Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha
Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili(MUHAS), Mamlaka ya Usimamizi wa
bandari za Tanzania(TPA), Mfuko wa Taifa wa
Bima ya Afya(NHIF), Taasisi ya Magonjwa ya Mishipa ya fahamu na Mifupa
(MOI), Shirikisho la viwango Tanzania (TBS) na Shirika la Utangazaji Tanzania
(TBC).
Sanjala na hayo Michezo ambayo itafanyika siku ni pamoja na
Mpira wa Miguu, Netiboli, Kuvuta Kamba, Ukimbia ukiwa na kijiko mdomoni kikiwa
na ndimu, Kukimbia ukiwa ndani ya gunia, Kukimbia huku ukitunga uzi kwenye Sindano,
kula pamoja na kukuna nazi kwa wanaume.
No comments:
Post a Comment