![]() |
| Kansela wa ujerumani Angela Merkel akichangia jambo mjini New york. |
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel
ameahidi kuwa Ujerumanin itatimiza wajibu wake wa kutenga asilimia 0.7 ya pato
kwa ajili ya kuendeleza kufadhili maendeleo
katika maeno mbalimbali.
Akizungumza katika hadhara Kuu ya Umoja wa Mataifa mjini New
York nchini Marekani jana, Merkel amehimiza nchi nyengine kutekeleza wajibu wao
ili watu wote duniani waweze kuishi maisha ya heshima.
Merkel aliongeza kuwa ni muhimu nchi zilizoendelea kiviwanda,
zitimize ahadi zao kama Ujerumani inavyoendelea
kuchangia dola bilioni 100 kwa nchi
zinazoendelea kuzisaidida kuhifadhi mazingira kuanzia mwaka 2020.
Merkel amesema kwa njia hiyo
wataweza kujenga Imani na kuleta maendeleo kwa ujumla, Merkel pia alizumgumzia
suala la wahamiaji barani Ulaya na kusema maelfu ya wahamiaji wanakimbia ugaidi
na vurugu katika nchi zao.
Aliongeza kuwa lazima dunia
ikabiliane na sababu zinazopelekea uhamiaji baada ya kumalizika kwa mkutano huwo wa siku
tatu, viongozi wakuu wa dunia wataanza mkutano mwengine Jumatatu ambapo
watazungumzia suala la uhamiaji barani Ulaya pamoja na vita
vinavyoendelea nchini Syria.

No comments:
Post a Comment