SIMBA NA YANGA LEO TABWE ? MGOSI ? KUONYESHA MAKALI YAO. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, September 26, 2015

SIMBA NA YANGA LEO TABWE ? MGOSI ? KUONYESHA MAKALI YAO.

Wachezaji wa Wekundu wa msimbazi Simba Sport Klabu.







Zikiwa zimebaki masaa machache kushuudia miamba ya soka hapa nchini simba na yanga ,ukiangalia katika michezo iliyopita  Kocha Muingereza wa Simba SC, Dylan Kerr  hakuwa na wachezaji wake wote wa kikosi cha kwanza kutokana na baadhi yao kuwa majeruhi, lakini ameweza kuiongoza timu kucheza vizuri na kushinda.

Mchezo wa kwanza dhidi ya Afrikani Sports safu yake ya ulinzi ilimkosa Nahodha Msaidizi, Hassan Isahaka, viungo Jonas Mkude, Abdi Banda na mshambuliaji Ibrahim Hajib.Isihaka na Hajib walipona na kucheza mchezo wa pili, wakati mchezo wa tatu aliwakosa beki mwingine tegemeo wa kati, Juuko Murushid na mshambuliaji mkongwe Mussa Hassan Mgosi.

Wachezaji wote hao wamefanya mazoezi katika kambi ya Unguja na wako fiti kuelekea mchezo wa leo- maana yake Kerr ana wigo mpana wa wachezaji kwa ajili ya mchezo dhidi ya Yanga Sc hii leo.

Ambapo  kikosi ambapo atakitumia leo ni pamoja na  Peter Manyika; Hassan Kessy, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Juuko Murushid, Hassan Isihaka, Justice Majabvi, Simon Sserunkuma, Said Ndemla, Ibrahim Hajib, Hamisi Kiiza na Mussa Hassan Mgosi, kinachoweza kuanza leo.
Lakini bado Kerr anaweza kuamua kutumia viungo watatu na kupunguza mshambuliaji mmoja. Tutaona muda ukifika.

Mshambuliaji  wa simba Mussa Hassan Mgosi
akiwa katika ubora wake


 




Na Kocha Mholanzi wa Yanga SC, Hans van der Pluijm amekuwa katika wakati mzuri mwanzoni mwa Ligi Kuu, kwani hana majeruhi na amekuwa akipanga vikosi vyake atakavyo katika mechi zake za awali.

Hakuwa na mabadiliko kutoka kikosi cha ushindi wa mechi ya kwanza, ya pili hadi ya tatu na sasa mashabiki wa Yanga SC wamekwishaijua kikosi cha kwanza  cha mwaka huu.

Mchezaji wa yanga  Amissi Tambwe









kikosi hicho ni pamoja Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Mwinyi Mngwali, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kelvin Yondan, Thabani Kamusoko, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Donald Ngoma, Amissi Tambwe na Godfrey Mwashiuya au Deus Kaseke. 


Lakini leo kunaweza kukawa na mabadiliko katika safu ya ulinzi, kutokana na taarifa za Nahodha Cannavaro kuumia mazoezini kisiwani Pemba hivyo Kuna wasiwasi pia, Niyonzima anaweza kuanzia benchi.

Haitakuwa ajabu leo, Barthez akianza pamoja na Juma Abdul kulia, Mwinyi kushoto, wakati katikati atalindwa na Twite na Yondan. Kamusoko amecheza vizuri mechi zote za awali, lakini leo anaweza kusogezwa juu, ili chini acheze Said Juma ‘Makapu’.


Benchi zima la ufundi likiongozwa  Hans van der Pluijm.









Kuna uwezekano pia Yanga SC ikaanza na viungo watatu, Salum Telela akiongezeka na kupunguza idadi ya mawinga, kwa sababu Simba SC ni timu yenye mtaji mzuri wa viungo.

MUSSA HASSAN MGOSI

Wachezaji wengi wamekuwa wakitajwa wiki yote hii kuelekea pambano la watani, kwa upande wa Simba SC, Hamisi Kiiza ‘Diego’ ndiye ameonekana kama mtaji mkubwa.

Lakini ukweli ni kwamba mtu hatari zaidi kwenye kikosi cha Simba SC kuelekea mchezo wa leo ni Mussa Hassan Mgosi, mchezaji mwenye uzoefu wa mechi za watani wa jadi kwa miaka 10 sasa.

Kama mchezaji, Mgosi ni fundi, hodari na mzoefu ambaye anawajua vizuri mabeki wa Yanga SC. Na zaidi Mgosi wa sasa si yule wa miaka mitatu iliyopita aliyekuwa anapenda kufunga mwenyewe tu- hapana huyu wa sasa anawatengenezea zaidi nafasi wengine.

Kiiza, Hajib na hata Awadh Juma wote, yeyote anaweza kutumbukiza mpira kwenye nyavu za Yanga SC, lakini mchezaji ambaye anatarajiwa kuwa na mvuto zaidi leo uwanjani kwa Simba SC, ni Mgosi. 

 AMISI JOSELYN TAMBWEM

ashabiki wa Yanga SC wameweka turufu zao zaidi kwa Donald Ngoma- kweli Mzimbabwe huyo ni hatari na anaweza kuwa tabu sana kwa Simba SC jioni ya leo.

Lakini mtu hatari zaidi kwa Simba SC leo ni Mrundi Amissi Joselyn Tambwe, ambaye hapana shaka kocha Hans van der Pluijm atamuanzisha kwa sababu anajua umuhimu wake awapo uwanjani.

Tambwe wa msimu huu, amekuwa anacheza kwa kuwafikiria kwanza wenzake kufunga na ndiye anaongoza hadi sasa kutoa pasi za mabao, lakini pia naye anafunga.

Tambwe amekutana na misukosuko mingi ya mabeki wa Tanzania na anawajua vizuri- isitoshe hao wa Simba SC amecheza nao anawajua kivitendo na maneno. Hakuna mtu wa kumtisha katika safu ya ulinzi ya Simba SC.

Uchezaji wa Tambwe umebadilika kwa kiasi kikubwa kutoka alivyokuwa Simba SC, na akiwa katika msimu wake wa pili Jangwani, tayari Mrundi huyo anajisikia yuko nyumbani.

YANGA MTEJA KWA SIMBA 

Tayari kuna imani, Yanga SC inaweza kushinda mechi yoyote ngumu, lakini si kwa Simba SC na hiyo ndiyo picha halisi kuelekea mchezo wa leo. Mashabiki wa Yanga hawana amani na timu yao kwa asilimia 100 mbele ya Simba SC.

Na Simba SC wanajiamini, wanaweza kufungwa na timu hata ya Daraja la Nne, lakini siyo Yanga SC. Simba SC wanaamini wanaweza kuifunga Yanga SC wakiwa na wachezaji wa aina yoyote.
Na kwa kiasi kikubwa hapo ndipo ulipolalia utamu wa mechi ya leo, kwamba baada ya uwekezaji wote katika usajili wa Yanga SC wataendelea kufanya vyema. 

HISTORIA SIMBA NA YANGA.Timu hizo mbili zimekuwa na upinzani mkubwa tangu zilipoanzishwa miaka ya 1935 na 1936,kitu ambacho kimechangia kuwepo uhasama mkubwa na kusababisha kugawana bara bara. 

Takwimu kuanzia timu hizo zilipoanza kukutana zinaonyesha Yanga ndiyo kinara kwa kupata ushindi mara nyingi zaidi ya Simba ambayo inafuatia kwa mbali. 

Takwimu kama hizo kwenye upande wa kunyakua ubingwa wa Tanzania bara pia zinaibeba Yanga kwa kuchukua ubingwa huo mara 25 wakati Simba ikifanya hivyo mara 18 na kufuatiwa na klabu za Mtibwa Sugar na Coastal Union ya Tanga. 

Rekodi nzuri kwa Simba katika mapambano yake na Yanga ni kupata ushindi wa mabao mengi kama ilivyofanya mwaka 1977 iliweza kuifunga Yanga mabao 6-0 na Mei 6 mwaka 2012 iliipa tena kipigo cha aibu cha mabao 5-0,uwanja wa taifa Dar es Salaam.

Simba imekuwa makini kwa kutumia vizuri madhaifu yawapinzani wao inapo wakuta wamechoka na kufunga mabao mengi yanayowapa rekodi nzuri kwenye historia za timu hizo. Takwimu za Goal za miaka sita iliyopita kuanzia 2009 zinaonyesha Simba na Yanga zimekutana mara 11 ikiwa ni mechi maalumu pamoja na zile za Ligi Kuu ya Tanzania bara. 

Katika idadi hiyo Simba inaongoza kwa kushinda mara nne na Yanga  ikipata ushindi mara tatu na mara nne zikienda sare lakini kizuri kwa Yanga ni kuwa na bahati ya kupata ushindi inapokutana na Simba mwezi Oktoba. 

Oktoba 16 mwaka 2010 pambano la Ligi Kuu Tanzania bara lilifanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0 mfungaji akiwa Jeryson Tegete dakika ya 70. 

Yanga ilifanya tena hivyo Oktoba 29/2011 kwa kuifunga Simba safari hii ikiwa  uwanja wa taifa Dar es Salaam mfungaji akiwa  Mzambia Davis Mwape dakika ya 75,na msimu uliofuata kidogo vijana wa Msimbazi waligoma kufanywa wateja baada ya kukutana Oktoba 3/2012 na kutoka sare ya 1-1 na Yanga   Simba wakitangulia kufunga kupitia kwa Amri Kiemba dakika ya tatu na Yanga ikasawazisha dakika ya 64 kupitia kwa Said Bahanuzi.  Oktoba  20,2013,Simba iligoma kwa mara nyingine kufungwa na Yanga kwenye mwezi huo baada ya kulazimisha sare ya mabao 3-3 huku yenyewe ikitoka nyuma ka mabao matatu yaliyofungwa kipindi cha kwanza na Yanga. 

Wafungaji wa Yanga katika mechi hiyo walikuwa ni Mrisho Ngasa aliyefunga bao la kwanza dakika ya 14 na Mganda Hamisi Kiiza aliyefunga mara mbili dakika ya 35 na dk47 . Mabao ya Simba yalifungwa na Beatram Mwombeki dakika ya 53Joseph Owino dakika ya 5 na Mrundi Gilbert Kaze dakika ya 83 mechi hii ikiwa maalumu ikipewa jina la Nani Mtani Jembe. 

Ushindi pekee iliyowahi kuupata Simba inapocheza na Yanga ndani ya miaka sita iliyopita ilikuwa ni Oktoba 31 ambapo iliweza kuifunga Yanga bao 1-0 mfungaji akiwa Mussa Hassani Mgosi dakika ya 26.

Katika takwimu hizi zilizowekwa na Mtandao wa Goal kila timu inacho cha kujivunia katika pambano leo imekuwa na kipindi kizuri katika miaka sita iliyopita wakati Yanga ikifurahi kukutana na Simba mwezi Oktoba kwa sababu imekuwa na bahati nao.


Rekodi nzuri kwa Simba katika mapambano yake na Yanga ni kupata ushindi wa mabao mengi kama ilivyofanya mwaka 1977 iliweza kuifunga Yanga mabao 6-0 na Mei 6 mwaka 2012 iliipa tena kipigo cha aibu cha mabao 5-0,uwanja wa taifa Dar es Salaam.

Simba imekuwa makini kwa kutumia vizuri madhaifu yawapinzani wao inapo wakuta wamechoka na kufunga mabao mengi yanayowapa rekodi nzuri kwenye historia za timu hizo.

Takwimu za Goal za miaka mitano iliyopita kuanzia 2009 zinaonyesha  Simba na Yanga zimekutana mara 11 ikiwa ni mechi maalumu pamoja na zile za Ligi Kuu ya Tanzania bara.

Katika idadi hiyo Simba inaongoza kwa kushinda mara nne na Yanga  ikipata ushindi mara tatu na mara nne zikienda sare lakini kizuri kwa Yanga ni kuwa na bahati ya kupata ushindi inapokutana na Simba mwezi Oktoba.  

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here