![]() |
| Mkuu wa umoja wa Mtaifa wa utoaji wa misaada ya binadam Stephen O'Brien akiwa katika majukumu yake ya kikazi. |
Mkuu wa Umoja wa Mataifa
anayehusika na utoaji wa misaada ya kibinadamu Stephen O'Brien anasema
ameshtushwa sana kwamba mashirika ya umoja huo yameamriwa kuondoka eneo la
Luhansk mashariki ya Ukraine kufikia leo na viongozi wa eneo hilo.
O'Brien alisema mashirika mengine yasiyo ya
kiserikali, likiwemo shirika la Madaktari wasio na Mipaka, yametakiwa yaondoke
Luhansk kufikia sept 26 mwaka.
Afisa huyo wa Umoja wa
Mataifa amesema agizo hilo ni ukiukaji wa sheria za kimataifa.
Aidha O'Brien alisema sera ya
waasi inahatarisha maisha, huenda
ikawaathiri watu zaidi ya milioni 3 kwa kuzingatia msimu wa baridi ukikaribia.
amesema operesheni za Umoja wa Mataifa katika
eneo la Donetsk mashariki ya Ukraine ziko hatarini kwa sababu shughuli za
mashirika yote ya umoja huo zimesitishwa.

No comments:
Post a Comment