Papa aliwasili Manhattan
baada ya safari fupi kutoka uwanja wa ndege wa John F. Kennedy kwa njia ya
helikopta.
Kiongozi huyo alihudhuria
ibada ya maombi kwa watu takriban 2,500 katika kanisa la Mtakatifu Patrick na katika
ratiba yake ya leo yenye shughuli nyingi Papa Francis atawahutubia viongozi
katika Umoja wa Mataifa na kushiriki ibada ya dini mbalimbali katika jumba la
makumbusho la mashambulizi ya Septemba 11, 2001 eneo la Ground Zero jijini New
York.
Akiwa new York ataongoza misa
katika uwanja wa Madison Square Garden na kutembea katika bustani ya katikati
ya mji huo.
Kiongozi huyo wa kanisa
Katoliki duniani aliwasili New York akitokea Washington ambako alilihutubia
bunge la Marekani na kuwahimiza wabunge wafanye juhudi zaidi kupambana na
ugaidi wa kimataifa.
Chanzo DW.

No comments:
Post a Comment