Miongoni
mwa changamoto hizo ni pamoja na kuchezewa madhambi na mchezaji mwezako jambo ambalo
linaonekana ni la kawaida
katika mchezo lakini wakati mwengine mchezaji umgalimu katika maswala mbalimbali ikiwemo katika utendaji na nafasi yake katika
kuhakikisha timu inapata matokeo.
Msomaji
wa Wingu la habari leo nakuletea orodha
ya wachezaji kadha ambao wamechezewa
madhambi mara nyingi kuliko wachezaji wengine unaowajua katika ramani
ya soko hapa duniania,
katika msimu mpya wa ligi ya Uingereza , na miongoni mwa wachezaji hao ni pamoja na mchezaji
wa West Ham UTD Mark Noble, huyu ndio mchezaji anayeongoza kwa kufanyiwa
madhambi katika ligi kuu Uingereza mpaka sasa.
Kwani amefanyiwa madhambi mara
19 katika michezo 6 aliyocheza tangu msimu mpya uanze, ukiwa ni wastani wa rafu
3.2 kwa mechi alizocheza.
Mchezaji wa pili Andre
Ayew wa Swansea ambaye amefanyiwa madhambi mara 18, ukiwa ni wastani wa
faulo 3 kwa kila mchezo.Wa
tatu ni Alexis Sanchez amefanyiwa mara 17 mpaka sasa kwa uwiano wa 2.8 kwa
mechi.
Eden
Hazard amefanyiwa mara 16 akiwa na uwiano
wa 2.7 kwa mechi, wakati Ross Barkley na
Sadio Mane wakiwa wamefanyiwa faulo mara 15, ukiwa ni uwiano wa 2.5 .
Na
mchezaji Idrissa Gueye wa Aston Villa
amefanyiwa madhambi mara 12, ukiwa ni wastani wa faulo 3 kwa kila mechi.
Historia inaonyesha kuwa msimu
wa mwaka jana, Eden Hazard ndio alikuwa mchezaji aliye fanyiwa faulo nyingi zaidi,
mara 113, ukiwa ni uwiano wa 3 kwa mechi.

No comments:
Post a Comment