JESHI LA POLISI WAJIPANGA KIKAMILIFU KUHAKIKISHA AMANI INATAWALA , MSHEZO WA SIMBA NA YANGA SEPT27 MWAKA HUU. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, September 25, 2015

JESHI LA POLISI WAJIPANGA KIKAMILIFU KUHAKIKISHA AMANI INATAWALA , MSHEZO WA SIMBA NA YANGA SEPT27 MWAKA HUU.












Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam limejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa pambano la mpira wa miguu kati timu za SIMBA na YANGA ambalo linavuta hisia za mashabiki wengi wa hapa Tanzania linafanyika katika hali ya amani na usalama.

Mchezo ambao unatarajia kufanyika katika dimba la taifa jijini dar es salaam  tarehe sept 27 mwaka huu,Hivyo mashabiki wanashauriwa wasiwe na shaka yoyote ya kiusalama lakini wanatakiwa kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa  za jambo lolote watakaloliona kuwa linaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani kwa kipindi chote watakapokuwa nje au ndani ya uwanja wa taifa.

Katika mchezo huo Kutakuwa na askari wa kutosha ambao watazunguka maeneo yote muhimu ya uwanja huo kwa lengo la kuimarisha ulinzi muda wote ambao uku askari wengine watakuwa katika milango mikuu ya kuingilia na ndani ya uwanja .

Sanjali na haya kutakuwa na ulinzi wa  kutumia camera (CCTV Camera) zitakazofungwa kuzunguka uwanja huo ili kusaidia kuimarisha ulinzi katika mechi hiyo muhimu, hivyo matukio yote yatakayokuwa yanatokea yatarekodiwa.




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here