RAIA WA MALI AFIKISHWA MAHAKAMANI BAADA YA KUFANYA UHARIBIFU NCHINI NIGER. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, September 26, 2015

RAIA WA MALI AFIKISHWA MAHAKAMANI BAADA YA KUFANYA UHARIBIFU NCHINI NIGER.

Raia mmoja wa Mali Ahmad Al Mahdi Al Faqi, amefikishwa mbele ya mahakama ya kimataifa ya uhalifu mjini  the Hague kwa madai ya kuhusika na uharibifu wa majengo ya kihistoria katika mji wa Timbuktu.
Al Faqi alisalimu amri nchini Niger wiki moja iliyopita baada ya kutolewa hati ya kukamatwa kwake.
Waendesha mashitaka wanamtuhumu Al Faqi kuwa ni mwanachama wa kundi la Ansar Dine, la Waislamu wa itikadi kali ambalo limeshikilia eneo kubwa la kaskazini mwa Mali tangu mwaka 2012.

Kundi hilo liliharibu majengo kadhaa ya kidini katika mji huwo wa kihistoria, ikiwa ni pamoja na makaburi ya mashekhe wakubwa wa dini ya Kiislamu

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here