BAABA YA KUCHEZEA KICHAPO KOCHA WA FC BARCELONA LUIS ENRIQUE ,ASEMA YAKE. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, September 24, 2015

BAABA YA KUCHEZEA KICHAPO KOCHA WA FC BARCELONA LUIS ENRIQUE ,ASEMA YAKE.

Fc Barcelona wamekubali kichapo cha mabao 4-1 dhidi ya celta vigo katika  La Liga uku wakiwa chini ya Luis Enrique siku ya Jumatano.
Kushindwa huko kumefikia kikomo cha rekodi yao ya kushinda mechi zao zote msimu huu.
Katika mchezo huo Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Iago Aspas alifunga mabao mawili baada ya Nolito kuanza kufunga mabao dhidi ya klabu hiyo yake ya zamani.
Neymar aliipatia Barcelona bao  moja la kufutia machozi zikiwa zimesalia dakika 10 kabla ya mchezo huo kuisha.
Barcelona walikuwa wamepoteza mechi moja pekee kati ya 25 walizocheza majuzi katika La Liga.
Ushindi wa Celta uliwaweka kileleni mwa ligi kwa muda, lakini Real Madrid waliwabandua baadaye baada ya kulaza Athletic Bilbao.
Kufatia matokeo hayo mkufunzi mkuu wa Barca Luis Enrique alisema kuwa Kilichoamua mechi hii ni jinsi ya  Celta walivyocheza vyema na kupata ushindi.
Aidha alisema kuwa katika mchezo walijalibu kushindana ulijaribu kushindana lakini waliwazidi  ujanja .
’’Timu inapokuwa bora na kukushinda, huwa huna mengi ya kusema,  hivyo heri nishindwe na timu inayocheza kama Celta walivyocheza leo, bila kutumia hila, kushinda kwa kucheza vyema soka, nawapongeza na natumai waendelee kucheza hivyo hivyo.”alisema
Kufungwa kwa Barcelona magoli manne ni mara ya tatu katika mechi tisa walizocheza msimu huu kwani Walilazwa 4-0 na Athletic Bilbao katika Super Cup ya Uhispania na pia walicharaza Sevilla 5-4 katika Super Cup ya Uefa.


                                                       

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here