Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene amevunja
bodi ya Soko la Machinga Complex lililopo Ilala Mchikini Dar es Salaam na
kulikabidhi kwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda.
Akizungumza katika mkutano wa
Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini (JWT), Simbachawene amesema wazo la
kuanzishwa kwa soko hilo lilikuwa zuri lakini Halmashauri ya Jiji la Dar es
Salaam imeshindwa kulitekeleza.
Jengo hilo lilikamilika kujengwa
mwaka 2010 likiwa na uwezo wa kuchukua wafanyabiashara 4206, lakini Waziri
Simbachawene alisema limeishia kuwa makazi ya popo.

No comments:
Post a Comment