Roger Federer kucheza na Martina Hingis Rio. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, December 12, 2015

Roger Federer kucheza na Martina Hingis Rio.

Mchezaji wa tenis Roger Federe mwenye furaha .



Nyota wa tenisi Roger Federer anatarajia kushirikiana na bingwa wa zamani wa Wimbledon Martina Hingis kutoka Uswizi katika mashindano ya jinsia mchanganyiko wa Michezo ya Olimpiki ya Rio 2016.
Federer, 34, na Hingis walicheza mara ya mwisho pamoja katika Kombe la Hopman nchini Australia 2001.
Bingwa huyo mara 17 wa Grand Slam amesema ana  kuwa anafuraha furaha sana”.
"Nilimuenzi sana nilipokuwa mchanga. Niliamini alikuwa na kipaji adimu,” aliongeza Federer, ambaye ni mdogo wa Hingis kwa mwaka mmoja.
“Tuko karibu sawa kwa umri na alikuwa akishinda mataji ya Grand Slam nilipokuwa bado kituo cha taifa cha tenisi. Nilishangazwa sana na ustadi wake.”
Image copyrightAPImage captionHingis alitwaa taji la Wimbledon mwaka 1997 akiwa na umri wa miaka 16
Hingis, 35, alishinda mataji matano ya Grand Slam katika uchezaji wake, moja akilitwaa Wimbledon mwaka 1997 akiwa na umri wa miaka 16.
Alikuwa amestaafu mara mbili awali lakini akarejea mchezoni tena 2013 na amekuwa akifanikiwa mashindanoni.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here