TWIGA STARS KUJIPIMA UBAVU NA MALAWI. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, September 23, 2015

TWIGA STARS KUJIPIMA UBAVU NA MALAWI.

Timu  ya taifa ya Wanawake ya mpira wa miguu Tanzania, TWIGA STARS inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya  timu ya Taifa ya Wanawake ya Malawi unaotarajiwa kupigwa   24 Oktoba mwaka huu nchini Malawi.

Akizungumzia mchezo huo wa kirafiki Msemaji wa Shirikisho la  mpira miguu TFF Baraka Kizibuto alisema kuwa mchezo wa Twiga Stars dhidi ya Malawi itachezwa jijini Lilongwe  baada kupata mwaliko wa chama cha soka nchini Malawi (FAM) kuialika Twiga Stars kwenda nchini Malawi kwa ajili ya mchezo huo.

Aidha amebainisha kuwa Mchezo huo wa kirafiki watatumia kama sehemu ya maandalizi ya vikosi vya timu zote mbili za Wanawake Tanzania na Malawi kwa ajili ya michuano mbalimbali .

Sanjali na hayo Mwenyekiti wa Chama cha Soka ya Wanawake Tanzania (TWFA), Amina Karuma anatarajiwa kuhudhuria kongamano la viongozi wa soka la wanawake duniania litakalofanyika Zurich nchini Uswisi Septemba 28 hadi  02 Oktoba mwaka huu.

Kongamano hilo linashirkisha viongozi 35 wanawake wa mpira wa miguu kutoka semehu mbalimbali duniani ikiwa ni muendelezo wa kongamano liliofanyika mwezi Machi mwaka huu nchini Canada wakati wa fainali za kombe la Dunia la Wanawake.





No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here