Kocha wa zamani wa Man Utd Alex Ferguson asema yake ya moyoni. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, September 23, 2015

Kocha wa zamani wa Man Utd Alex Ferguson asema yake ya moyoni.

Meneja wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson kabla ya kuachia  mikoba klabuni  hapo alitaka mshahara wake uongezwe maradufu baada ya mshahara wa Wayne Rooney kuongezwa mwaka 2010.
Rooney alikuwa ametishia kuhama United lakini mwishowe akatia saini mkataba wa kulipwa ujira wa £250,000 kila wiki.
"Niliwaambia sikudhani ilikuwa haki kwa Rooney kulipwa mshahara mara mbili ya mshahara wangu,” Ferguson amesema kwenye kitabu kipya.
Aidha mwenyekiti mwenza wa Man United Joel Glazer alisema kuwa  walikubaliana Roney  lakini hakuwa zamila yao kufanya hivyo.
'haikuwa  rahisi, tuliamua kuendelea naye kwa sababua  hakuna mchezaji anayefaa kulipwa mshahara mkubwa kunishinda.”
Kwenye kitabu chake kipya kuhusu usimamizi chenye jina la Leading , Ferguson anasimulia kuhusu kipindi cha mpito alipoondoka Manchester United 2013 baada ya kuwa kwenye usukani miaka 26, akisema: "Tungeliisimamia vyema.”
Raia huyo wa Scotland, aliyeshinda mataji mawili ya Ligi ya Kilabu Bingwa Ulaya, mataji 13 ya Ligi ya Premier, vikombe vitano vya FA na vikombe vinne vya League, alirithiwa David Moyes, aliyefutwa miezi 10 baadaye.
Lakini mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 73 anasema alitaka pia kuzungumza na aliyekuwa kocha wa Barcelona ambaye sasa ananoa Bayern Munich Pep Guardiola kabla yake kumteua Moyes.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here