Dr Ali Mohamed Shein aweka mipango yake bayana, Visiwani Zanzibar. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, September 22, 2015

Dr Ali Mohamed Shein aweka mipango yake bayana, Visiwani Zanzibar.

MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Ali Mohamed Shein amesema atahakikisha Zanzibar inajitosheleza kwa chakula na kupunguza uagizaji wa chakula nje ya nchi, kwa kuimarisha kilimo cha umwagiliaji mpunga mashambani.
Dk Shein alisema hayo Tunguu katika Wilaya ya Kati Unguja wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni na kusema wakati umefika kwa Zanzibar kujitosheleza kwa chakula na kupunguza uagiziaji chakula nje ya nchi ambao unaligharimu taifa fedha nyingi za kigeni.
Alizitaja juhudi zilizochukuliwa hadi sasa ni kuanzishwa kwa mashamba darasa 1,200 ya mpunga ambapo tani 674,334 za mazao ya chakula zimezalishwa ukilinganisha na tani 346,535 katika mwaka 2014, ongezeko hilo limefikia asilimia 95.
Alifafanua kuwa jumla ya matrekta 45 yamenunuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) huku matrekta makongwe 37 yakifanyiwa matengenezo makubwa pamoja na mashine za kuvuna mpunga 14 zikinunuliwa.
Aidha, alisema eneo la uzalishaji mpunga limeongezeka kutoka hekta 10,000 mwaka 2010 na kufikia hekta 34,000 mwaka huu huku akisisitiza kwamba kiwango cha uzalishaji wa mpunga kimeongezeka kutoka tani 20,000 hadi tani 33,655 pamoja na kuongezeka kwa idadi ya kaya zinazozalisha kilimo hicho na kufikia 10,000 mwaka 2010 hadi kufikia 70,000 mwaka 2014.
“Hizo ndizo juhudi zetu na mipango yetu katika kuimarisha kilimo cha umwagiliaji mashambani cha mpunga na kuona kwamba tunapunguza uagiziaji nje ya nchi kwa kuwawezesha wakulima wetu,” alisema Dk Shein anayeomba muhula wa pili na mwisho wa urais Zanzibar.
Alisema malengo yamewekwa hadi kufikia 2017- 2018, asilimia 60 ya mahitaji ya kilimo cha mpunga kiwe kinazalishwa nchini ambapo mabonde ya mpunga yaliyopo Cheju, Mtemela Pemba yataimarishwa.

Alieleza kuwa matumaini yapo makubwa zaidi baada ya serikali kuchukua juhudi za kuimarisha Kituo cha Kilimo cha Kizimbani kwa kupokea idadi kubwa ya wanafunzi wa cheti kutoka 300 katika mwaka 2010 hadi kufikia 741 katika mwaka 2014 huku mafunzo ya Stashahada katika fani ya uzalishaji mifugo na uzalishaji wa mazao ya kilimo mjumuishi yameanza kufundishwa kwa wanafunz.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here