WAZIRI MWIJAGE AWAPA FURSA WAMILIKI WA VIWANDA KUSHIRIKI MAONYESHO YA PILI YA DIDHAA DESEMBA 7 MWAKA HUU. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, November 30, 2017

WAZIRI MWIJAGE AWAPA FURSA WAMILIKI WA VIWANDA KUSHIRIKI MAONYESHO YA PILI YA DIDHAA DESEMBA 7 MWAKA HUU.


Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe Charles Mwijage akizungumza na waandishi wa habari jijini leo Dar es Salaam.

Na Noel Rukanuga.
Wizara ya Viwanda na Uwekezaji kupitia Mamlaka ya Maendeleoa ya Biashara Tanzania (Tan Trade) imewataka wamiliki wa viwanda vidogo, kati na vikubwa kushirikia katika maonyesho ya pili ya bidhaa za viwanda yanayotarajia kufanyika Desemba 7 hadi 11 mwaka huu.

Maonyesho hayo yatafanyika katika viwanja vya maonesho ya biashara wa mwalimu J.K Nyerere (sabasaba) vilivyopo barabara ya kilwa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Charles Mwijage, amesema kuwa zaidi ya viwanda 500 wanatarajia kushiriki katika maonyesho ya mwaka huu.

Amesema kuwa kwa mwaka huu idadi ya washirikiki inatarajiwa kuongezeka kutokana katika kipindi cha miaka miwili kuna viwanda vipya 3,306 ambavyo vinauwezo wa kuajili zaidi ya watu 10.

Mhe. Mwijage amefafanua kuwa katika monyesho ya mwaka wa jana kulikuwa na makampuni 472 pekee ambayo yalishiriki.

“Lengo la maonesho ni kuwaweka wadau wa viwanda pamoja ili wapata fursa ya kujadiliana, kubadilisha uzoefu wa kuzalisha bidhaa pamoja kuuza nje ya nchi,”amesema Mwijage.

Amesema kuwa maonesho hayo mwaka huu yanabeba kauli mbiu isemayo “Tanzania sasa tunajenga viwanda” ikilenga kuwaaminisha wananchi juu ya falsafa na dhima ya ujenzi wa viwanda wa uchumi wa viwanda.

Amesema kuwa meonesho hayo yatawakutanisha wadau wa viwanda ikiwemo wazalishaji wa malighafi, taasisi zinazotoa huduma mbalimbali kwa wenye viwanda na taasisi zinazowezesha wenye bidhaa kutoka kiwandani mpaka kufikia kwa mtumiaji.

Amesema wakati wa maonesho desemba 11, 2017 itakuwa siku maalumu ya viwada Afrika ambayo itaratibiwa na kwa ushirikiano na Taasisi za Umoja wa Mataifa ya Maendeleo ya Viwanda (UNIDO).

Mhe. Mwijage amesema wizara yake kupitia Mamlka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade) imewakaribisha watanzania wanaomiliki viwanda vidogo, vya kati na vikubwa kushiriki maonesho hayo.

Katika hatua nyengine amewataka wafanyabiashara kuanza wakiwa na mitaji midogo ili waweze kuendelea na kuapata fursa ya kukuza uchumi kupitia viwanda. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here