MAHAFALI YA KUMI CHUO CHA KODI YAFANYIKA, WAHITIMU WAFUNDWA - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, November 18, 2017

MAHAFALI YA KUMI CHUO CHA KODI YAFANYIKA, WAHITIMU WAFUNDWA

Baadhi ya wahitimu yaliofanyika  
novemba 18, 2017
Na Noel Rukanuga.
Zaidi ya Wahitimu 500 wa Chuo Cha Kodi (ITA) wametakiwa kutumia vema elimu waliopata chuoni hapo katika kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa kulipa kodi kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

Akizungumza katika Mahafali ya Kumi ya Chuo Cha kodi (ITA) Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dkt. Yamungu Kayandabila, amesema kuwa ni vema wanafunzi kuwa wazalendo kwa kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya maendeleo ya taifa. 

Dkt. Kayandabila ambaye ni mgeni rasmi katika Mahafali hayo ambapo alimwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mapango, amesema “Serikali itaendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi katika chuo cha kodi kwa kuongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ili taifa liwe na maendeleo”.

Hata hivyo amewataka wahitimu hao kuendelea na masomo katika ngazi nyengine ili kuongeza mahalifu katika masula ya kodi jambo ambalo linaweza kuleta chachu ya maendelo katika jamii.

Katika hatua nyengine amebainisha kuwa serikali itaendelea kushirikiana na chuo kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kuhakikisha chuo hicho kinapiga hatua na kuwa msaada kwa kuzalisha wanafunzi wenye vigezo.

“Chuo kina nafasi kubwa ya kuendelea na udahili wanafunzi wengi kwa maendeleo ya taifa” amesema Dkt Kayandabila.

  
Mkuu wa Chuo Cha Kodi (ITA) Profesa Isaya Jairo, amewataka wahitimu kwenda kuwa mabalozi kwa kukitangaza chuo vizuri kupitia taaluma zao.

Amesema kuwa kufanya hivyo itasaidia kuleta maendeleo kwa watanzania kuwa na mwamko wa kulipa kodi.

Hata hivyo Prof Jairo ameeleza kuwa miongoni mwa changamoto zinazowakabili chuoni ni pamoja na baadhi ya wanafunzi wanashindwa kuendelea na masomo kutokana na ukosefu wa fedha na kusababisha kushindwa kumudu gharama za chuo.

“Baadhi ya wanafunzi wameshindwa kumaliza chuo kutokana na kukosa ada, hivyo tunaiomba serikali kutoa mikopo idadi kubwaya wanafunzi wetu” amesema prof Jairo.

Prof Jairo amewataka wahitimu hao kwenda kutatua changamoto ambazo wanakwenda kukutanz nazo ikiwemo ukosefu wa ajira.

Amesema kuwa wahitimu hao hawapaswi kukaa nyumbani ila wanapaswa kutumia elimu yao kutengeneza fursa za ajira.

Aidha amefafanua kuwa chuo kinatoa fani fupi na ndefu katika katika masula ya kodi kuanzia ngazi ya cheti na kuendelea.

Amesema katika kuleta maendeleo chuo hapo, Chuo kina Baraza la Uongozui ambapo kazi yao kutoa ushauri katika masula mbalimbali ya kitaalamu chuoni hapo. 
Hata hivyo ametoa zawadi mbalimbali kwa wahitimu 12 waliofanya vizuri zaidi katika masomo ikiwa ni utaratibu ambao chuo kimejiwekea ili kutambua jitihada nzuri ambazo zimefanywa na wanafunzi hao pamoja na kuwashajihisha wanafunzi wanaoendelea na masomo kufanya vizuri zaidi katika masomo. 

Katika fani mbalimbali zinazotolewa katika chocha kodi jumla ya wanafunzi waliotunukiwa vyeti, stashahada na shahada katika mahafali ni wahitimu 82 wa Cheti cha Uwakala wa Forodha cha Afrika Mashariki yaani the ‘East African Customs and Freight Forwarding Practising Certificate (EACFFPC). 


Wahitimu 39 wa Cheti cha Usimamizi wa Forodha na Kodi yaani ‘Basic Technician Certificate in Customs and Tax Management (CCTM).


Stashahada ya Usimamizi wa Forodha na Kodi yaani (Diploma in Customs and Tax Management  (DCTM)) ni wahitimu 147.

Shahada ya Usimamizi wa Forodha na Kodi yaani (Bachelor of Customs and Tax Management (BCTM) ni wahitimu 134.

East African Community Postgraduate Certificate in Customs Administration (PGCCA) ni wahitimu 85 na Stashahada ya Uzamili katika Kodi yaani (Postgraduate Diploma in Taxation (PGDT) wahitimu ni 33.

Pamoja na kutunuku vyeti stashahada, na shahada kwa wahitimu, mgeni Rasmi alitoa tuzo kwa wahadhiri wa Chuo cha Kodi waliofanya tafiti mbalimbali katika kipindi cha mwaka wa masomo wa 2016/2017 na kuchapishwa katika majarida mbalimbali ya kitaaluma, ikiwa ni pamoja na jarida la Chuo cha Kodi yaani ‘Journal of the Institute of Tax Administration’ (JITA).


Hata hivyo chuo hicho kinasherehekea miaka kumi tangu kipate ithibati (usajili) kutoka Baraza la Taifa la Vyuo vya Ufundi (NACTE).


Chuo cha kodi kinajivunia miaka kumi ya mafanikio katika kutoa mafunzo ya Forodha na Kodi yanayokidhi soko la ajira katika nyanja za forodha na Kodi ndani na nje ya nchi.

Tangu kipate usajili wa kudumu kutoka Baraza la Vyuo vya Ufundi (NACTE), Chuo kimepanua wigo wa taaluma kutoka kutoa mafunzo kwa watumishi wa TRA pekee hadi kutoa mafunzo kwa wadau mbalimbali wa masuala ya forodha na kodi kwa nchi za Mashariki Kati na Kusini mwa Afrika. 

Kikiwa katika hatua za mwisho za utekelezaji wa Mkakati wa tatu, Chuo cha Kodi kinaendelea na maandalizi ya kuwa Kituo cha Umahiri wa Forodha na Kodi katika ukanda wa Afrika Mashariki baada ya Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kukiteua Chuo cha Kodi kuwa Kituo cha Umahiri Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here