Ukiukwaji wa haki za watoto umeongezeka 2015 - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, June 3, 2016

Ukiukwaji wa haki za watoto umeongezeka 2015

Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa imesema ukiukwaji wa haki za watoto katika maeneo yaliyo na vita umeongezeka mwaka uliyopita, hususan nchini Afghanistan, Syria, Yemen, Iraq, Somalia pamoja na Sudan Kusini.
Ripoti hiyo ya kila mwaka kuhusu watoto katika maeneo ya vita imesema tangu Umoja wa Mataifa ulipoanza kuweka kumbukumbu ya vifo vya raia na majeruhi mwaka 2009,  idadi kubwa zaidi ya watoto waliojeruhiwa imerikodiwa nchini Afghanistan.
Ripoti hiyo imeeleza kuwa maelfu ya watoto ni miongoni mwa watu 250,000 waliouawa nchini Syria. Na nchini Yemen idadi ya watoto wanaotumiwa katika vita na pande zinazopigana imeongezeka mara tano mwaka jana ikilingamnishwa na mwaka juzi.

Aidha nchini Somalia ukiukwaji wa haki za watoto umeongezeka kwa asilimia 50. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here