![]() |
Mkemia mkuu wa
serikali Profesa Samwel Manyere akizungumza na waandishi wa habari kuhusu
vigezo vya uingizaji Kemikali.
|
WINGU
LA HABARI
Wafanyabiashara
wanaongiza Kemikali nchini pasipo kufata utaratibu wapigwa marufuku kuigiza kemikali
hizo hadi pale watakapofata sheria na kanuni zilizopo.
Mbali
na kufata sheria zilizopo, wafanyabiashara hao wametakiwa kuingiza mizingo hiyo
ikiwa na label yenye lugha ya Kiswahili au kiingereza kama ilivyoelekezwa
kwenye jedwali la 19 katika kanuni za Sheria ya Usimamizi na Udhibiti.
Akizungumza
na Waandishi wa Habari -, Profesa Samwel Manyele amesema kuwa sheria inamtaka
anayeingiza kemikali nchini lazima aweze amesajiliwa.
Profesa
Manyele amesema kuwa sehemu ya tatu ya sheria kwa kuzingatia kifungu cha 11-28 inamtaka
mfanyabiashara awe amepewa hati ya usajili (Certificate of Registration) kama
ilivyobainishwa kwenye kifungu cha 29 kabla ya kuanza kujishughulisha na
biashara.
Amefafanua
kuwa sehemu ya pili ya kanuni za Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali ya
mwaka 2015, kanuni ya 3(1) (e) inaelekeza kila mdau wa kemikali aliyesajiliwa na
kupata hati ya usajili inapaswa kuomba kibali cha kuingiza kemikali nchini.
“Wafanyabiashara
wengi wamekuwa na utaratibu wa kuagiza kwanza mizigo na inapowasili ndipo
wanaaza kuomba kubali lakini ni kinyume cha sheria” amesema Profesa Manyele.
Hata
hivyo amebainisha kuwa miongoni mwa changamoto zilizopo ni pamoja na kuingiza
mizigo kabla ya kuomba kibali na kusababisha mrundikano wa mzigo bandarini
inayosubiri vibali na ukaguzi.
Amesema
kuwa wadau wengi wamekuwa na uelewa mdogo wa kisheria na kanuni zake kutokana
na kuwatumia Mawakala wa forodha (Agents) bila wao wenyewe kufika kwa ajili ya
kuonana na watendaji wanaotoa vibali na ukaguzi.
Profesa
Manyele amesema licha ya changamoto zilizopo lakini wanaendelea kuwaelimisha
wadau kuhusiana na matakwa ya sheria na kanuni zake juu ya uingizaji wa
kemikali nchini kutoka nje ya nchi.
Mwisho.

No comments:
Post a Comment