Nidhamu katika Matumizi ya Fedha, Ni chanzo cha mafanikio ya kiuchumi. - WINGU LA HABARI- ONLINE

Breaking

TANGAZO

TANGAZO
Sugar free

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Sunday, October 18, 2015

Nidhamu katika Matumizi ya Fedha, Ni chanzo cha mafanikio ya kiuchumi.



Habari za wakati huu msomaji wa wingu la habari, bila shaka nina imani  enaendelea vizuri na kama kuna matatizo basi mimi naendelea kukuombea ili uweze kukabiliana na changamoto ambazo kwa namna moja hama nyingine zinakufanya kutokamilisha mipango yako kwa wakati.
Kama kawaida kila siku ya Juma pili uwa nakuletea Makala ya uchumi lengo ikiwa ni kukumbushana kipi ambacho unatakiwa kufanya katika sekta ya uchumi  na kutimiza malengo yako kwa wakati, kwani asilimia kubwa ya watu ususani vijana wanapopata fedha wanashindwa kufanya mambo ya kimaendeleo na kujikuta wanatumia katika matumizi ambayo sio ya lazima kwao.
Katika maisha ya kila siku tunayoishi nidhamu ni kitu bora , na leo nitazungumzia nidhamu ya matumizi ya fedha na kukufanya kufanikiwa katika maisha yako katika maswala ya  kiuchumi, nidhamu katika matumizi ya fedha ndiyo nguzo pekee inayoweza kumfikisha mtu kwenye kiwango cha mafanikio anachokitaka, hata kama kipato cha mtu huyo ni kidogo kiasi gani, hivyo kufikia malengo aliyojiwekea.
Bila shaka uliwahi kuwaona watu wawili wanaofanya kazi katika kampuni moja, wakifanya kazi moja na kulipwa mshahara sawa, lakini wakawa na mafanikio tofauti, kwa mmoja wao kuweza kujenga nyumba yake ya kisasa ya kuishi yeye na familia yake huku mwenzake akiendelea kupanga chumba mjini, huku wote wakiwa na ukubwa wa familia ulio sawa.
Na wakati mwengine  umewahi kuwaona watu wawili wanaofanya kazi katika kampuni moja, wakifanya kazi moja na kulipwa mshahara sawa, lakini mmoja wao ana miradi yake nje ya kazi au kutafuta vyanzo vingine vya kumwingizia kipato nje ya muda wa kazi, huku mwingine akisubiri tu mshahara wake wa mwisho wa mwezi kama kwamba kwake bila mshahara hakuna maisha.
Kitu gani kinawatofautisha kimaendeleo watu hao wawili wakati wote wanalipwa stahiki zinazofanana, lakini  Kubwa linalowatofautisha hapa ni nidhamu ya matumizi ya fedha  katika mpangilio wa matumizi yao kutokana na mshahara wao wa mwezi.
Msomaji wangu leo nakuletea nguzo nne za kuyafikia malengo ya mafanikio kiuchumi katika maisha. Nguzo hizo nne ni nidhamu katika matumizi ya fedha, kufanya kazi kwa bidii na kujituma, kutoa huduma bora kwa wateja na upekee na ubunifu unaweza kuhimili ushindani katika soko.

Hivyo leo tutazungumzia nguzo moja  ya kwanza inayohusu nidhamu katika mpangilio na matumizi ya fedha.Kwani  kuna wajasiriamali wengi tu wanaofanya biashara ya kuuza mchicha, sukuma wiki, mnafu ,matunda na kadhalika.
Aidha, kuna wafanyakazi walioajiriwa katika taasisi kubwa kama vile serikalini, mashirika ya umma na makampuni binafsi makubwa.
Lakini, katika makundi haya mawili, kundi la wajasiriamali waunza mboga mboga na kundi la wafanyakazi walioajiriwa katika taasisi kubwa, unaweza kukuta huyu anayeuza mboga akiwa anamiliki nyumba nzuri, anasomesha watoto wake katika shule nzuri, na halafu huyu aliyeajiriwa na kupata mshahara kwa mwezi akawa hana hata kibanda, huku akiwa haishiwi na madeni yanayotokana na mikopo.
Nini kinatokea kwa kwa wawili hao wakawa na tofauti hiyo ya maisha, Jibu ni moja tu. Mmoja wao ana nidhamu ya fedha, mwingine hana nidhamu hiyo wala hana malengo yoyote kuhusu maisha yake.
Bila nidhamu ya fedha ni vigumu kufanikiwa kimaisha. Watu wengi wameshindwa kusonga mbele kiuchumi, na badala yake kujikuta wakidumaa kiuchumi kwa sababu ya kukosa nidhamu hiyo. Watu wa aina hii, maisha yao yote, miaka nenda rudi, yanakuwa ni yale yale, hayabadiliki kwa kuwa na hali nzuri.
Siri ya mafanikio ipo katika kila jinsi unavyoipangilia na kutumia kila senti moja inayopita mikononi mwako. Ni muhimu kwa yeyote mwenye nia ya kufikia malengo fulani ya kiuchumi, kujitathimini ni kwa vipi anatumia kila senti inayopita mkononi mwake. Je, sehemu ya kila senti hiyo inayopatikana, inawekwa akiba ili iongezeke ama inatumika kuzalisha senti nyingine au anaitumia mara moja na kusahau?
Kutokuwa na nidhamu ya fedha kumewasababishia baadhi ya watu kufilisika na kugeuka kuwa ombaomba, pamoja na kwamba kabla ya kufilisika walikuwa na fursa hata ya kwenda kukopa fedha kwenye taasisi za fedha.
Katika dunia ya sasa, bado kuna baadhi ya watu wamegeuka kuwa watumwa wa maisha kutokana na tabia yao ya kutaka kujionyesha kwa watu kwamba wanazo fedha za kutumia, hata kama fedha hizo wanazipata kwa shinda.
Kwa hakika kabisa, watu wa aina hii, hufika mahali wakayajutia maisha yao pindi kipato hicho wanachokichezea leo kutokana na kutokuwa na nidhamu ya fedha kuyeyuka, kwa sababu tu ya kuhendekeza starehe.
Wanasahau kwamba katika dunia ya sasa, heshima ya mtu inakuwepo kutokana na mafanikio aliyonayo mtu kiuchumi, hasa ushiriki wake kikamilifu katika shughuli za kijamii zinazohusiana na maendeleo yao kwa ujumla.
Hata hivyo, msingi mkuu wa nidhamu ya fedha ni familia. Wazazi hawana budi kuwa mfano bora wa nidhamu katika matumizi ya fedha kwa watoto wao ili nao, kwa kuiga mfano wa maisha ya wazazi wao, waweze kufanikiwa kiuchumi.
Mimi ninaamini yeyote anayeamua kuchukua hatua sasa, kwa kuthubutu kubadilisha tabia yake juu ya nidhamu katika matumizi ya fedha zake, mafanikio katika maisha yanapatikana kwa njia ya mteremko tu. Fanya uamuzi sasa ili uwe kati ya miongoni mwa watu waliofanikiwa kiuchumi.

Mwiki ijayo nitazungumzia nguzo ya pili ambayo  ni Kufanya kazi kwa bidii na kujituma.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here