| Meneja masoka la hissa Patric Mususa, akitoa taarifa ya wiki juu ya soko hilo jijini Dar es Salaam |
Idadi ya mauzo katika
soko la hissa Dar es salaam (DC) imeshuka kutoka bilioni 106 kwa wiki iliyopita
hadi kufikia bilioni 2.5 kwa wiki hii.
Akizungumza na wingu la habari jijini Dar es salaam Meneja
wa soko hilo Patric Mususa alisema kuwa katika soko hilo pia idadi ya hissa
zilizonunuliwa na kuuzwa imeshuka kutoka milioni 8 hadi kufukia milioni 1.4 kwa
wiki hii .
Alisema kuwa Kampuni tatu zinazoongoza katika soko hissa
zake kununuliwa na kuuzwa ni CRDB BAKI, TBL, TCC, kwani CRDB BAKI inaongeza kwa 90%, wakati TBL
ikiwa na 5.8% uku kampuni TCC ikiwa na
asilimia 1.17.
Mususa amebainisha kuwa mtaji katika soko hilo imepungua kwa wastani kutoka tirioni 22.5 hadi
tirioni 22.2,uku idadi ya mtaji wa kamupuni za ndani ikishuka kutoka tirioni
9.8 hadi 9.7.
Hata hivyo amezitaja Kampuni tatu zinazongoza hissa zake
katika bei ni pamoja na Uchumi supermekert ikiwa na asilimia nne , kenya airway
asilimia nne uku kampuni ya T way gases ikiwa na asilimia 1.3.
Sanjali na hayo alisema kuwa Kiashiria cha soko upande wa kibeki
na fedha imeshuka kwa nukta 34 kikiwa kimechangiwa kwa kiasi kikubwa kushuka kwa
mauzo katika kampuni ya CRDB na NMB, na katika sekta ya viwanda pia kimeshuka
kwa nukta nne ikiwa imechangiwa kwa kushuka kwa mauzo katika kampuni ya TBL na
Twiga cement.
‘’Kwa ujumla kiashiria cha soko kimeshuka kwa wastani ya
nukta 16 ingawa soko linaoneka kuwa katika kiwango kizuri licha ya kushuka kwa asimilima 98 kwa wiki
hii, kwani kushuka uko kumechangiwa na Serikali wiki iliyopita kuja kununua na
kuuza hissa yake ambazo waliwekeza muda mrefu’’ alisema.
Hata hivyo amebainisha kuwa katika upande wa kununua na
kuuza hissa kwa njia ya simu wameendelea kupata mwitigio mzuri na kuwataka watu
wengine waendeele kujiunga na huduma hiyo kwa kupiga namba *150*36# ambayo
inayojulikana kwa jina DS MOBILE TRADE kwani mpaka sasa wameongezeka watu kutoka 600
hadi kufukia watu 700 katika huduma hiyo.
No comments:
Post a Comment